Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi akitia saini
mkataba wa ushirikiano wa kutoa huduma na mafunzo kati ya JKCI na
Hospitali ya Moyo ya BLK ya India. Kulia ni mwakilishi wa Hospitali ya
Moyo ya BLK ya India akitia saini kuhusu mkataba huo.
Taasisi
ya Moyo ya Jakaya Kikwete –JKCI- kwa kushirikiana na Hospitali ya BLK
kutoka nchini India kwa mara ya kwanza imefanya upasuaji mkubwa wa moyo
kwa kupandikiza mishipa ya damu kwenye moyo (Buypass Surgury ) bila
kuusimamisha moyo kwa kutumia mashine maalum inayoitwa Heart Lung
Machine.
Upasuaji huo ni mkubwa wa kwanza na wa aina yake kufanyika hapa nchini na kwa kanda Afrika ya Mashariki na Kati .
Akizungumza
na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam , Kaimu Mkurugenzi wa
Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Dk. Peter Kisenge amesema wataalam wa
taasisi hizo mbili kwa mara ya tatu wameweza kutoa tiba kubwa ya moyo
bila mgonjwa kupasuliwa kwa kutumia mtambo wa Cathlab kwa kuzibua Valvu
zilizoziba( BMV Procedure ).
Wataalam
hao wa Moyo ambao watakuwa hapa nchini kwa siku mbili watatoa mafunzo
kwa watoa huduma wa Taasisi ya moyo ambapo wagonjwa watakaopewa huduma
hii watafikia takribani 18 .
“
Taasisi itaokoa zaidi ya Shilingi Milioni 180 kwa siku mbili kama
wagonjwa hawa wangepelekwa nje ya nchi kwa matibabu haya haya , na kubwa
zaidi si fedha tu bali tumeokoa maisha ya watanzania wenzetu” amesema
Dk. Kisenge.
Katika
hatua nyingine, Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete imetia saini mkataba
wa ushirikiano wa kutoa huduma na mafunzo na Taasisi ya BKL ya nchini
India , lengo ni kuwapa mafunzo watumishi wake na kuendelea kutoa huduma
ya upasuaji wa moyo kwa kushirikiana na taasisi ya BLK .
Kwa
mwaka huu peke yake JKCI imefanya procedure 471 ikiwemo upasuaji wa
Moyo kwa kufungua kifua 99, vipandikizi 78 , vizibua njia 265 na
nyinginezo 29 .
Mbali
na ushirikiano huu na Taasisi ya BLK , JKCI imeweza kufanikisha huduma
hizi kubwa kwa kushirikiana na taasisi nyingine marafiki zikiwemo
Al-Muntada ( Saudi Arabia ) Open Heart International ( Australia) , Save
a Child’s Heart ( Israel) na Madaktari Afrika.
Kambi kama hizi zitaendelea tena Julai, Septemba na Novemba .
Kaimu
Mkurugenzi wa Huduma za Tiba katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete
(JKCI), Dk Peter Kisenge akizungumza na waandishi wa habari leo baada ya
taasisi hiyo kufanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa moyo wa kupandikiza
mishipa ya damu. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Profesa
Mohamed Janabi na Mwenyekiti wa Hospitali ya Moyo ya BLK ya nchini
India, Dk Subhash Chandra. Watu 18 watafanyiwa upasuaji wa njia hiyo kwa
kushirikiana na wataalamu kutoka India.
Mwenyekiti
wa Hospitali ya Moyo ya BLK nchini India, Dk Subhash Chandra
akizungumza na waandishi wa habari leo kuhusu upasuaji mkubwa wa moyo
unaofanyika JKCI. Kulia ni Mwenyekiti wa Hospitali ya Moyo ya BLK ya
India, Dk Ajay Kaul.
Kaimu
Mkurugenzi Huduma za Upasuaji JKCI, Dk Bashir Nyangasa akiwaeleza
waandishi wa habari jinsi walivyofanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa
moyo kwa kutumia njia ya upandikizaji mishipa baada ya mishipa hiyo
kutolewa sehemu ya miguuni ya mgonjwa. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi
Mtendaji wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi na Mwenyekiti wa Hospitali ya
Moyo ya BLK ya India, Dk Subhash Chandra.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni