MKURUGENZI Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), Godfrey Simbeye amesema kuwa urasimu mkubwa uliopo katika kusimamia masuala ya uwekekezaji umechangia kuwakimbiza wawekezaji.
Alisema hayo mwishoni mwa wiki wakati akizungumza katika Baraza la Biashara la Mkoa wa Kigoma. Alisema uchunguzi uliofanywa na taasisi yake umebaini Tanzania inapoteza fursa nyingi za uwekezaji kutoka nje ya nchi kutokana na mazingira ya urasimu na rushwa.
Simbeye alisema kuwa urasimu huo pia umekuwa ukilalamikiwa na Mabalozi wanaoiwakilisha nchi katika nchi mbalimbali ulimwengu ambao licha ya uhamasishaji mkubwa wanaoufanya, wameishia kupata lawama kutoka kwa wawekezaji waliofika Tanzania kutokana na urasimu waliokumbana nao.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni