Ndugu
wasomaji wetu, kama tulivyosoma kwamba maumivu ya mama mwenye mimba
huwa ni makubwa na ndiyo maana popote kwenye maumivu huwa kuna mapenzi
ya kweli.Kama tunavyoamini kwamba upendo wa bwana wetu yesu kristu kwetu
unadhihirika pale msalabani,ndivyo maumivu anayoyapata mama mjamzito
ndivyo mapenzi yanavyokuwa makubwa.Kwahiyo kama hukusikia maumivu wakati
wa kujifungua basi amini mtoto huyo humpendi kama wengine..by baba
profa hahah....Furaha ya mama inaanza pale anapokabidhiwa mtoto wake
baada ya kujifungua
UWEPO WA BABA WAKATI WA KUJIFUNGUA. Baadhi
ya familia hawakubaliani nami kwamba ni vyema baba kuwepo katika tukio
la kujifungua lakini kwakweli kwa maoni yangu ni vyema baba akashiriki
kikamilifu yale mapenzi ya mama kwa mtoto. Kwanza inampa nguvu mama
ajisikie kwamba hayuko pekeyake.Ni mda huu huwa nawahurumia akina mama
wanaochukuwa mimba bila kujua ni nani kampatia mimba hiyo maana muda huu
huwa wako peke yao na manesi wenye hila.
FURAHA YA BABA HUWA NI SAWA NA YA MAMA
Ni maumbile tu yanayo tofautisha furaha ya
mama na ile ya baba kwani ya baba uambatana na huruma kubwa sana na
ndiyo maana baadhi ya wababa hawapendi kuwepo kwenye tukio kwasababu ya
kutotaka kuona machungu anayo yapata mama.Na wengine wanashindwa kushika
kichanga kwani ukihurumia kwamba labda watakiumiza.Furaha ya baba na
mtoto ni sawa na ya mama na mtoto.Wapendwawasomaji,kuweni na christmas
njema na mwaka mpya
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni