.

.

22 Julai 2015

SPIKA WA BUNGE AMEWAONGOZA MAMIA YA WAKAZI WA DODOMA KATIKA KAZISHI YA MH MARIAM MFAKI










 

Spika wa bunge Mhe Anne Makinda ameongoza mamia ya wakazi wa mji wa Dodoma katika kumuaga na kumzika aliyekuwa mbunge wa viti maalum CCM mkoa wa Dodoma marehemu hajat Mariam Mfaki aliyefariki dunia jumanne hii kwenye hosipitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma kutokana na kuugua na maradhi ya saratani ya damu kwa muda mrefu.
Katika risala yake kwa waombolezaji spika Anne Makinda amemuelezea marehemu hajat Mariam Mfaki kuwa alikuwa kiongozi muwajibikaji ambaye alitumia muda mwingi kushughulikia matatizo ya wananchi na kuyafikisha katika sehemu husika bungeni.

Akisoma risala ya marehemu kwa niaba ya katibu wa bunge mkurugenzi msaidizi huduma kwa wabunge Suleiman Mvunye amesema kabla ya marehemu kuwa mbunge alifanya kazi mbalimbali za kuhudumia jamii akianzia na afisa maendeleo wizara ya tawala za mikoa na serikali za mitaa kuanzia mwaka 1965.

Mbali na ubunge wa viti maalum marehemu pia aliwahi kushika wadhifa wa katibu wa umoja wa wanawake Tanzania UWT na mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM NEC wilayani humo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni