.

.

15 Aprili 2016

MH.ADRIAN TIZEBA AHAMIA RASMI CHAMA CHA MAPINDUZI


Image result for CCM LOGO
Aliyekuwa Mwenyekiti wa chama cha Demokrsaia  na Maendeleo Chedema mkoa wa Mwanza Andrian Tizeba, leo amejiunga rasmi na CCM wilayani  Sengerema tawi la Lugata.

Tizeba ambaye alitangaza kujivua uanachama wa chadema Machi 29 mwaka huu baada ya kusimamishwa uongozi kwa muda wa mwaka mmoja, na kutangaza kuachana na siasa, amekabidhiwa kadi hiyo  na katibu wa tawi hilo Alfred Mwambala.

Akizungumza kwa njia ya simu, Tizeba amesema uamuzi wake si wa kulazimishwa na mtu bali, ameona ni vema arudi kwenye chama chake cha awali.

Tizeba ambaye ni kaka wa mbunge wa jimbo la Buchosa, Charles Tizeba amesema, nia na dhumuni la kujiunga na chama hicho ni kutokana na utendaji wa Rais John Magufuli anaoufanya.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni