.

.

26 Aprili 2016

MKUU WA WILAYA IRINGA ATUMIA SIKU YA MUUNGANO KUSIKILIZA KERO ZA WANAKIJIJI WA MUGABIKE.

      Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akizungumza na wanakijiji wa Magubike

Sikukuu ya Muungano nimesherekea kwa kwenda Kijiji cha Magubike kusikiliza kero za wana kijiji. Tumefanikiwa kutatua kero nyingi na zingine ikiwa ni suala la bajeti mfano changamoto ya uchakavu wa miundo mbinu ya maji pamoja na ujenzi wa Bwawa kubwa ambalo upembuzi yakinifu tayari. (zianhitajika 2.5B). Mkutano wa leo pia nilisuruhisha ugomvi mkubwa kati ya Mwenyekiti wa kijiji na aliyekuwa Mwenyekiti wa ITCOJE Bwana Msafiri Pamagila. Wanannchi walifurahi sana kwani watu hawa wote ni maarufu pia wana wafuasi wengi. Tunashukuru Mungu tumemaliza salama. Pia namshukuru Mzee Nyangalima kwa maneno ya busara. Shukrani kubwa zimwendee Diwani wa kata Mh Steven Mhapa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Iringa pia Makamu Mwenyekiti wa ALAT.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni