.

.

31 Machi 2015

NIGERIA WATAKIWA KUKUBALI MATOKEO YA UCHAGUZI


 
Taasisi za kieneo na kimataifa zimewataka wanasiasa na wananchi wa Nigeria kukubali matokeo ya uchaguzi yanayotarajiwa kutolewa na Tume ya Uchaguzi ya nchi hiyo.
Hii ni katika hali ambayo tume hiyo imesema kuwa, matokeo ya awali ya uchaguzi mkuu uliofanyika siku ya Jumamosi yatatangazwa kesho Jumanne. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon amesema uchaguzi wa Nigeria kwa kiwango kikubwa ulifanyika kwa utulivu na mpangilio wa kuridhisha. Mkuu huyo wa UN amesema kuna haja kwa Wanigeria kuonyesha ukomavu wa demokrasia kwa kukubali matokeo yatakapotangazwa. Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Magharibi mwa Afrika (ECOWAS), imetoa kauli kama hiyo na kusisitiza umuhimu wa kudumishwa amani nchini Nigeria hata baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa.

Kiti cha urais kiliwavutia wagombea 14 ingawa mchuano mkali umetajwa kuwa kati ya Rais wa sasa, Goodluck Jonathan na kiongozi wa zamani wa kijeshi, Mohammadu Buhari.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni