.

.

31 Machi 2015

WANANCHI SIMANJIRO WAPINGA ZOEZI LA KUPIMA MIPAKA



Zoezi la kuweka mipaka mipya ya mkoa wa manyara na Dodoma mipaka ambayo pia inadaiwa kusababisha mgogoro wa muda mrefu kati ya kijiji cha KIMOTOROK na pori tengefu la mkungunero limeshindikana baada ya wakazi wa kijiji cha KIMOTOROK kulikataa zoezi ilo kwa madai kuwa tume ya wataalam wanayofanya kazi hiyo hawakushirikishwa na mipaka inayowekwa imeingia ndani ya kijiji chao hivyo hawapotayari kuona zoezi hilo likiendelea.
Wakizungumza na ITV baada ya kugomea zoezi ilo na wapimaji kuondoka katika eneo ilo wakazi wa kijiji cha KIMOTOROK wamesema wameshindwa kuvumilia kuona zoezi hilo likiendelea huku wapimaji kutoka serikalini wakiendelea kupotosha kwa kuweka mipaka ndani ya kijiji chao na wananchi wakikatazwa kushiriki na kwamba zoezi hilo linampango wa kuongeza mgogoro siyo kumaliza.
Mwenyekiti wa kijiji cha KIMOTOR Elias Ormonyo amesema awali
Alipatiwa taarifa kuwa wapima watakuja katika eneo hilo lakini
Walipofika hakushirikishwa na cha ajabu hata yeye mwakilishi wa
Mwananchi htakiwi kujua kinachoendelea hivyo anaunganana
Wananchi kulikataa zoezi hilo.
Mbunge wa simanjiro CHRISTOPHER OLE SENDEKA ameeleza masikinitiko yake kwa namna zoezi hilo ambalo lingeweza kuwa utatuzi wa mgogoro kushindikana na kuitaka serekali kuwa makini inapo tekeleza mipango yenye maslahi kwa wananchi na iwashirikishe kwakuwa wananchi wanayajui maaeneo yao kuliko mtaalam anayefika kwa mara ya kwanza.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni