.

.

07 Juni 2015

MAKAMU WA RAIS ATEMBELEA BOHARI YA KUHIFADHI MAFUTA YA GBP MKOANI TANGA


1Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Msimamizi wa Kituo cha kupokelea mafuta cha Kampuni ya GBP, wakati alipokuwa katika ziara yake ya kutembelea Jeti ya kupokelea mafuta na Bohari ya kuhifadhia mafuta ya kampuni hiyo, wakati alipokuwa katika ziara yake ya siku moja mkoani Tanga jana Juni 5, 2015.

2
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiondoka katika eneo hilo baada ya kukagua kituo hicho cha kupokelea mafuta cha Kampuni ya GBP, mkoani Tanga jana.
4
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongoizana na baadhi ya viongozi wa Kampuni ya GBP, wakati akielekea kukagua Bohari ya kuhifadhia mafuta ya Kampuni ya GBP, alipokuwa katika ziara yake ya siku moja mkoani Tanga jana.
5
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya GBP, Badar Seif Sood, (wa pili kulia) wakati alipotembelea Bohari ya kuhifadhia mafuta ya kampuni hiyo, kwenye ziara yake ya siku moja mkoani Tanga jana.
6
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiondoka katika eneo hilo, akiongozana na Mkurugenzi wa ya GBP, Badar Seif Sood (kushoto), Waziri wa Mazingira wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Binilith Mahenge na baadhi ya viongozi, baada ya ukaguzi wa Bohari ya kuhifadhia mafuta ya Kampuni ya GBP, mkoani Tanga jana.
7
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Mkurugenzi wa Kampuni ya GBP, Badar Seif Sood, baada ya kumaliza ziara yake ya kukagua Bohari ya kuhifadhia mafuta ya kampuni hiyo, jana mkoani Tanga.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni