.

.

14 Machi 2016

NAIBU WAZIRI "JAFFO" ATOA AGIZO KUHUSU SOKO JIPYA LA KIMATAIFA LA MWANJELWA, MBEYA



NAIBU  Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Suleiman Jaffo. wapili kutoka kushoto akiwa ameongoza na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Nyilembe Munasa wa( kwanza kulia) Kaimu Mkurugenzi wa Jiji Dk Samweli Lazaro wa (tatu kutoka kulia) na Meya wa Almashauri wa( nne kutoka kulia ) Mh David Mwashilindi. wakimpitisha maeneo Mbalimbali ya soko Jipya la Mwanjelwa.(Picha na David Nyembe wa Fahari News)



NAIBU  Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Suleiman Jaffo akikagua Vyoo kaktika Soko la Mwanjelwa. (Picha na David Nyembe wa Fahari News)


Mwonekano wa Soko Jipya la Mwajelwa.

NAIBU  Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Suleiman Jaffo akiangalia maeneo Mbalimbali ya Soko la Mwanjelwa na kusalimiana na wafanyabiashara amabo tayari wameanaza kufanya Biashara zao ndani ya Soko hilo la Kisasa la Mwanjelwa




NAIBU  Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Suleiman Jaffo, ameiagiza halmashauri ya Jiji la Mbeya, kuhakikisha inaliimarisha soko jipya na la kisasa la Mwanjelwa ili liwe kivutio kwa wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi.
Amesema, endapo soko hilo litaenda vizuri, watu wote kutoka nchi mbalimbali hususani nchi za kusini mwa afrika, watakuwa wanaishia hapo na kuendesha shughuli zao.
Jaffo, aliyasema hayo juzi wakati akitembelea na kukagua Soko hilo la Mwanjelwa ambalo ujenzi wake umegharimu zaidi ya shilingi Bilioni 20 zilizotolewa kwa mkopo kutoka benki ya CRDB.
Amesema, kama viongozi watakuwa na mikakati madhubuti na yenye tija samabamba na kutanguliza uzalendo, Soko hilo litakuwa ni kitovu cha biashara, na ndani ya miaka mitano kunawatu watakuja kujifunza hapo.
“Hivi karibuni nilibahatika kusimamia uchaguzi wan chi za nje kama mbili hivi, Zimbabwe na Zambia lakini nilijionea wafanyabiashara wa hapo wakiendesha shughuli zao kwa kutumia malighafi kutoka Tanzania tena kutoka Soko la Kariakoo,”amesema.
Amesema, hivyo kama viongozi watajipanga vizuri, watakuwa wameiweka nchi kwenye nafasi nzuri ya kibiashara na nchi kuwa miongoni mwa Taifa linaloenda kwa kasi kiuchumi.
“Hakuna miujiza kwa hili, jambo la msingi ni watu kuwa wazalendo, kutumia vizuri rasilimali tulizokuwa nazo tena kwa uadilifu mkubwa,”alisema.

               credit Fahari News

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni