.

.

23 Machi 2016

TCRA YAWATAKA WANANCHI KUTOA MALALAMIKO SEHEMU HUSIKA.

MUN1Na Jacquiline Mrisho- MAELEZO
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imewataka wananchi wenye malalamiko yanayohusu huduma zitolew
azo na makampuni ya simu kutosita kupeleka malalamiko yao kwenye makampuni husika.
Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Bw. Innocent Mungy ameyasema hayo leo jijini Dar es salaam katika mahojiano maalumu alipokua akijibu swali kuhusu malalamiko ya wananchi juu ya huduma zinazotolewa na makampuni mbalimbali ya simu hapa nchini.
Amesema mteja ana wajibu wa kujua matumizi na gharama za huduma za mitandao anazotumia pia ana haki ya kutoa malalamiko kwa kampuni husika ili aweze kupatiwa majibu na endapo hatasikilizwa anaruhusiwa kuwasiliana malalamiko yake Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania
Bw. Mungy ameongeza kuwa,wananchi wanaweza kufikisha malalamiko yao TCRA kwa kupiga simu au kutuma ujumbe mfupi kwenda namba 0784558270 au barua pepe;malalamiko@tcra.go.tz na malalamiko hayo yatafanyiwa kazi haraka.
Aidha, amefafanua kwamba,TCRA haipangi bei elekezi kwa makampuni hayo hivyo gharama za mawasiliano ziko kwenye mifumo mbalimbali kutegemeana na gharama za uendeshaji wa huduma kwenye kampuni husika.
 “Mwananchi halazimishwi kutumia huduma ya mtandao mmoja wa simu ana uhuru wa kuchagua na kutumia mtandao wowote wenye unafuu kwake” Amesisitiza.
Amewaomba wananchi waelewe kwamba soko la makampuni ya simu limekuwa na ushindani mkubwa jambo linaloyalazimisha makampuni yanayotoa huduma kubuni ofa mbalimbali kwa lengo la kuvutia wateja.
“ Sasa hivi soko la makampuni ya simu limekuwa na ushindani mkubwa nchini, jambo linalofanywa na makampuni hayo ni kuweka ofa mbalimbali ambazo hizo huwasaidia wananchi kupunguza gharama za matumizi ya simu”

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni