.

.

02 Aprili 2016

MBEYA CITY FC YAIBUKA NA USHINDI WA MAGOLI MANNE KWA SIFURI DHIDI YA COASTAL UNION



Mbeya city fc yaibuka na ushindi wa magoli manne kwa sifuri dhidi ya Coastal Union kutoka Tanga katika uwanja wa sokoine mjini Mbeya,ambapo mpira ulianza kwa kasi huku timu zote mbili zikiwa zinashambuliana.
Goli la kwanza la timu ya Mbeya city fc lilifungwa mnamo dakika ya 3 ya mchezo kupitia kwa Salvatory Nkulula,ambapo uzembe wa golikipa wa Coastal union aliweza kuigharimu timu yake baada ya kuutema mpira uliopigwa kwa adhabu.
Mpira uliendelea kwa kasi yakushambulina kipindi chote cha kwanza cha mchezo na goli hilo lilidumu kwa kipindi chote cha kwanza mpaka pale timu ya Mbeya city fc walipopata goli la pili dakika ya 57 ya mchezo kupitia kwa Salvatory huku akipokea pasi nzuri kutoka kwa Hassani Mwasapili na kuipatia timu ya Mbeya city fc goli la pili.
Mchezo safi uliooneshwa na timu zote mbili huku ukiwa unashuhudiwa na mgeni rasmi waziri wa habari,utamaduni,sanaa na michezo Mh Nape Moses Nnauye pamoja na mkuu wa mkoa wa Mbeya Mh Amos Gabriel Makalla.
Goli la tatu lilipatikana mnamo dakika ya 74 likifungwa na Hassan Mwasapili ambapo aliweza kuwainua mashabiki wa timu ya Mbeya city fc baada ya kupiga kwa ufundi mkubwa na mpira kuingia moja kwa moja katika nyavu za timu ya Coastal union,huku goli la nne likiwekwa nyavuni dakika ya 87 kupitia kwa Ditram Nchimbi na kukamilisha jumla idadi ya magoli manne Mpaka dakika 90 zinamalizika Mbeya city fc nne Coastal Union sifuri na mpaka sasa Mbeya city fc inafikisha pointi 27ikicheza michezo 25 huku Coastal union akishikilia mkia wa ligi kuu Tanzania bara akiwa na pointi 19 akicheza michezo 25.
Huku waziri wa habari,utamaduni,sanaa na michezo Mh Nape Moses Nnauye akisisitiza katika michezo si sehemu ya kuleta mambo ya chama pamoja na mambo mengine amabayo yanaweza kudidimiza michezo katiaka nchi ya Tanzania.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni