.

.

21 Juni 2016

MATUKIO KATIKA PICHA KUTOKA BUNGENI MJINI DODOMA LEO



Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiteta jambo na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mh. George Masaju leo Bungeni Mjini Dodoma. 
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Harrisom Mwakyembe akijibu moja ya hoja zilizotolewa Bungeni leo na Mbunge wa Nchemba Mhe. Juma Nkamia aliyetaka kujua uhalali wa mtuhumiwa aliyetenda kosa la jinai la kumtukana Rais kuachiwa huru na kwenda kutafuta fedha za kulipa faini ilihali kosa alilotenda limemdhalilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli. 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Uratibu Bunge Walemavu Vijana Kazi na Ajira, Mhe. Jenista Mhagama akiteta jambo na Mbunge wa Mtera Mhe. Livingstone Lusinde leo Bungeni Mjini Dodoma. 
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson akijibu miongozo iliyoombwa na wabunge mapema leo Bungeni mjini Dodoma kabla ya Kuahirisha shughuli za Bunge leo Mjini Dodoma. Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kisasa ya mjini Dodoma wakiwa katika ukumbi wa Bunge kwa lengo la kujifunza majukumu ya Bunge leo Mjini Dodoma wakati wa kipindi cha maswali na majibu. 
Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Dkt. Susan Kolimba akifafanua kuhusu hatua zinazochukuliwa ili kuimarisha Balozi za Tanzania katika nchi mbalimbali ikiwa ni moja ya hatua za kuimarisha uhusiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na mataifa mbalimbali. 
Naibu Waziri Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla akijibu maswali yaliyoulizwa na Wabunge leo Bungeni juu ya mikakati ya Serikali kuwawezesha wanawake kupitia Benki ya wanawake kwa kufungua madirisha maalum Katika Mikoa mbalimbali hapa Nchini yatakayosaidia kuwasogezea wanawake huduma za Benki hiyo ili waweze kujikwamua kiuchumi. Wanafunzi wa chuo Kikuu Dodoma (UDOM) Wakiwasili katika ukumbi wa Msekwa Bungeni Mjini Dodoma leo kwa lengo la kujifunza jinsi Bunge linavyotekeleza majukumu yake.
PEP GUARDIOLA APANDISHA PRESHA MASTAA MANCHESTER CITY A+ A- Print Email KOCHA mpya wa Manchester City, Pep Guardiola anatarajiwa kutua wiki ijayo na sasa swali kubwa lililopo ni je, atambakisha staa yupi? Pia wengi wanajiuliza iwapo ataendelea kumuamini Vincent Kompany kuwa nahodha wake na je, atafanya kazi tena na nahodha wa Ivory Coast, Yaya Toure au atamuuza? Ikumbukwe Guardiola alifanya kazi na Toure kwenye klabu ya Barcelona, lakini akamuuza kuja City miaka mitano iliyopita na mchezaji huyo akaleta neema ya mataji Etihad. Hata hivyo, swali lisilo na majibu kwa sasa ni je, wawili hao watafanya kazi pamoja hasa ikizingatiwa kuwa, Tore kila mara amekuwa akilalamika kutoheshimiwa ndani ya klabu hiyo. Kama hiyo haitoshi, Guardiola anasubiriwa kuamua hatima ya baadhi ya mastaa ambao mikataba yao inaelekea ukingoni huku baadhi yao umri pia ukianza kuwatupa mkono. Miongoni mwa mastaa ambao wanasubiri kocha huyo aamue hatma yao ni pamoja na kiungo Samir Nasri, beki Bacary Sagna, Wlfried Bony, Eliaquim Mangala na Aleksandar Kolarov. Wengine ni mshambuliaji wa Hispania, Jesus Navas, mlinzi wa kutegemewa wa Algentina, Pablo Zabaleta, Mfaransa Gael Clichy, Fabian Delph, Nicolas Otamendi, Fernando, Sergio Aguero na kipa anayetishia mara kadhaa kutaka kuondoka Joe Hart. Kikosi hicho ghali zaidi katika soka la Uingereza kilionekana kuwa tishio katika Ligi Kuu England kabla ya kuanza kwa msimu uliopita, lakini baadae kikaonekana si chochote wlolote baada ya kumaliza katika nafasi tatu.

Soma zaidi hapa >>: http://www.saluti5.com/2016/06/pep-guardiola-apandisha-presha-mastaa.html#more
Copyright © saluti5
PEP GUARDIOLA APANDISHA PRESHA MASTAA MANCHESTER CITY A+ A- Print Email KOCHA mpya wa Manchester City, Pep Guardiola anatarajiwa kutua wiki ijayo na sasa swali kubwa lililopo ni je, atambakisha staa yupi? Pia wengi wanajiuliza iwapo ataendelea kumuamini Vincent Kompany kuwa nahodha wake na je, atafanya kazi tena na nahodha wa Ivory Coast, Yaya Toure au atamuuza? Ikumbukwe Guardiola alifanya kazi na Toure kwenye klabu ya Barcelona, lakini akamuuza kuja City miaka mitano iliyopita na mchezaji huyo akaleta neema ya mataji Etihad. Hata hivyo, swali lisilo na majibu kwa sasa ni je, wawili hao watafanya kazi pamoja hasa ikizingatiwa kuwa, Tore kila mara amekuwa akilalamika kutoheshimiwa ndani ya klabu hiyo. Kama hiyo haitoshi, Guardiola anasubiriwa kuamua hatima ya baadhi ya mastaa ambao mikataba yao inaelekea ukingoni huku baadhi yao umri pia ukianza kuwatupa mkono. Miongoni mwa mastaa ambao wanasubiri kocha huyo aamue hatma yao ni pamoja na kiungo Samir Nasri, beki Bacary Sagna, Wlfried Bony, Eliaquim Mangala na Aleksandar Kolarov. Wengine ni mshambuliaji wa Hispania, Jesus Navas, mlinzi wa kutegemewa wa Algentina, Pablo Zabaleta, Mfaransa Gael Clichy, Fabian Delph, Nicolas Otamendi, Fernando, Sergio Aguero na kipa anayetishia mara kadhaa kutaka kuondoka Joe Hart. Kikosi hicho ghali zaidi katika soka la Uingereza kilionekana kuwa tishio katika Ligi Kuu England kabla ya kuanza kwa msimu uliopita, lakini baadae kikaonekana si chochote wlolote baada ya kumaliza katika nafasi tatu.

Soma zaidi hapa >>: http://www.saluti5.com/2016/06/pep-guardiola-apandisha-presha-mastaa.html#more
Copyright © saluti5

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni