.

.

31 Machi 2015

UPDATES: TAARIFA YA NYONGEZA/UFAFANUZI YA TUKIO LA KULA NJAMA NA KUJARIBU KUMTOROSHA ASKOFU JOSEPHAT GWAJIMA AKIWA HOSPITALI


jana tarehe 30/03/2015 waandishi wa habari walifika kituo Kikuu

cha Polisi wakitaka kujua uhalali wa silaha iliyokamatwa tarehe 

29/03/2015. Silaha hiyo ni Bastola aina ya BERRETA yenye 
namba CAT5802 ikiwa na risasi tatu. Pia zilikamatwa risasi 17 za 
Short Gun. 


Ufafanuzu ni kama ifuatavyo: 

Uchunguzi wa kina na wa kitaalam sasa umethibitisha kwamba 

silaha hiyo inamilikiwa kihalali na Askofu Josephat Gwajima. 
Kuhusu risasi 17 za Short Gun ni kwamba Askofu Gwajima 
anamiliki Bunduki aina ya Short Gun yenye namba 102837 
ambayo inatumia risasi za aina ya hizo zilizokamatwa. 





Kuhusu watu 15 wanaotuhumiwa kujaribu kumtorosha Askofu 

Josephat Gwajima bado uchunguzi unaendelea. Aidha watu hao 
pia wanahojiwa kuhusu suala la kukutwa na silaha na risasi 
zilizotajwa hapo juu wakati wao sio wamiliki halali za silaha hiyo 
na risasi hizo na idadi iliyotajwa kwa mujibu wa sheria.


Baada ya uchunguzi wa suala hilo jalada la kesi litapelekwa kwa 

mwanasheria wa Serikali kabla hawajafikishwa mahakamani ili 
sheria ichukue mkondo wake.


KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM,

S. H. KOVA,

DAR ES SALAAM.

Tupe Maoni Yako( Usiandike Matusi )

Sakata la mwanafunzi aliyekutwa amekufa ndani ya shimo la majitaka limechukua sura mpya baada ya wananchi wenye hasira kali kuchukua sheria mkononi baada kuvunja na kuichoma moto nyumba. Tazama ilivyo anzwa kuchomwa moto Tatizo la kujichukulia Sheria mkononi limeendelea kuwa kubwa kwa jamii ya watanzania, katika sakata la hivi karibuni ambapo baadhi ya watu walikuvunja na kuichoma moto nyumba ya mkazi mmoja wa mtaa mbwile b jijini Mbeya kwa tuhuma za kubaka na kumuua mwanafunzi wa miaka nane. Nyumba ikiwa imebomolewa Katika hali isiyo ya wakawaida wakazi hao wamejikuta wakichukua sheria mkononi kwa kuivunja na kuichoma moto nyumba ya Mariamu kasonta baada ya kumtuhumu mlinzi wake kumbaka mwanafunzi wa darasa la pili katika shule ya msingi majengo mwenye umri wa miaka nane jina limehifadhiwa na kisha kumkuta akiwa ameuwawa na kutupwa katika shimo la maji taka. Wakazi hao ambao walipimga vibaya mlinzi huyo aliejulikana kwa jina moja la Charles ambae alikamata siku ya tatu tangu kutokea kwa tukio hilo na kuokolewa na askali polisi waliowahi kufika katika eneo la tukio, wananchi hao walivamia nyumba ya bosi wake kisha kuibomoa na kuchoma moto ambapo kikosi cha zimamoto kilifika na kufaninikiwa kuuzima moto huo kabla ya kuiteketeza nyumba hiyo kabisa. Askali wa jeshi la polis baada ya kufanikiwa na kuwadhibiti wananchi kiatika kutekeleza uharifu huo Mwenyekiti wa mtaa mzee Bukuku akiwataka wakazi wa eneo hilo kuondoka na kuacha kuibomoa nyumba hiyo, Zunda gabliel kaimu mkuu wa kituo cha polisi kati akiongea na wananchi kufanya ulinzi wa nyumba iliyokua ikibomolewa Henry kakobe askali wa kata ya Nonde akiwatuliza wananchi katika mkutano ulioitishwa na mwenyekiti wa mtaa huo. Wananchi waliofika kwenye mkutano wakitaka mtu aliehusika na mauwaji ya mwanafunzi atajwe. Askali kanzu wakiimalisha ulizi katika mkutano wa wananchi wa Nonde Mbeya Rebeka mwalyego afisa mtendaji wa mtaa wa mbwile (b) akiongea na waandishi wa habari katika eneo la tukio

Copy and WIN : http://ow.ly/KfYkt

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni