.

.

19 Mei 2015

MAKAMPUNI YA MAFUTA YATAKIWA YATOSHELEZE SOKO LA NDANI - PINDA


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda ameyataka makampuni yanayojihusisha na mafuta na gesi nchini, kuhakikisha yanatimiza mahitaji ya Soko la Ndani na ukanda wa Afrika Mashariki kabla ya kufikia Soko la Nje.
Aliyasema hayo jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Utafiti na ufunguzi wa kozi ya Shahada ya Uzamili ya Mafuta na Gesi za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Katika hotuba iliyosomwa na Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene alisema Tanzania na Ukanda wa Afrika Mashariki bado una mahitaji makubwa ya rasilimali ya gesi hususani katika viwanda na nyanja zote.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni