.

.

19 Mei 2015

WABUNGE WALIA NA RUSHWA OFISI ZA UMMA

!
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Celina Kombani.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Celina Kombani.
KUKOSEKANA kwa Sheria ya kutenganisha biashara na uongozi ili kuweka nidhamu kwa viongozi wa umma kumesababisha kuwepo na mmomonyoko mkubwa wa maadili kwa viongozi hao, ambao wamekuwa wakitumia ofisi za umma kwa maslahi binafsi, hivyo kufanya vitendo vya rushwa kukithiri.
Wakichangia mjadala wa hotuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma bungeni jana, wabunge mbalimbali walisema ukosefu wa sheria hiyo umesababisha kuwepo kwa mianya mingi ya rushwa inayofanywa na baadhi ya watumishi wa umma.
Akichangia hoja hiyo, Mbunge wa Manyoni Mashariki, John Chiligati (CCM) alisema hivi sasa kuna mmomonyoko mkubwa wa maadili na baadhi ya viongozi wa umma hutumia ofisi za umma kwa maslahi binafsi.

credit mjengwa blog

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni