.

.

15 Septemba 2015

YWCA MBEYA WAMUWAGA RASIMI AFISA MRADI WA WAJIBIKA.

                                  Rebeka Njulumi akizungumza na wadau wa YWCA Mbeya.

          wadau mbalimbali wakiwa katika sherehe fupi yakumuwaga Rebeka Njulumi.

                Rebeka(katikati) akikabidhiwa cheti cha ufanyaji kazi kwa bidii
                                        Picha zote na Robert Eliah

YWCA Mbeya wamuwaga Rebeka Njulumi ambaye alikuwa afisa mradi wa wajibika Mkoani mbeya,sherehe hiyo fupi yakumuwaga Rebeka ilifanyika katika ofisi za YWCA zilizozopo eneo la Mabatini,nakudhuriwa na watu mbalimbali pamoja na wadau wa YWCA Mbeya.
Kwaa upande wake afisa msaidizi wa mradi huo bwana Elly Bonkey aliweza kumshukuru Rebeka kwa kipindi chote walichokuwa nae katika kuhakikisha wananchi wanatunza mazingira na kupanda miti,lakini pia aliweza kumshukuru kwa kutoa elimu ya vikoba kwa kina mama wa maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mbeya.
Nae mwanafunzi wa Nzonda haki Mussa Mbugi ambaye ni mwenyekiti wa mradi wa wajibika shuleni hapo aliweza kumshukuru Rebeka kwa kuwafanya wae mfano bora wa utunzaji mazingira shuleni hapo hususani kupanda miti na kuweka mazingira katika  hali ya usafi.
Katiaka upande wa kinanamama ambao waliweza kupata elimu ya vikoba waliweza kumshukuru Rebeka na kumtaka huko aendako akaendeleze mapambano ya kuwatoa watu katika umasiki na kuwapa elimu ya vikoba ili mradi tu watu wakima cha chini wanufaike na elimu anayoitoa.
















       

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni