Taarifa kutoka Uhispania zinasema kuwa nyota Mbrazili na Klabu ya
Barcelona zinasema kuwa amekubali kujiunga na klabu la mabingwa wa
Ufaransa (PSG) mwaka 2017.
Taarifa kutoka kwenye gazeti la Uhispania AS, "Neymar amekutana na
mmiliki wa klabu hiyo Al-Nasser Al-Khelaifi huko Ibiza wiki chache
zilizo pita. PSG wako tayari kutoa kitita cha pound million 153 kwa
ajili ya Neymar ili nyota huyo asiweze uongeza mkataba pale Nou Camp
ambapo mkataba wake unaisha mwaka 2018."
Neymar ana marafiki zake PSG – Marquinhos, Thiago Silva, David Luiz,
Lucas Moura na Maxwell. Pia makubaliaono hayo yataweza kuzidiha kipato
chake mara mbili mpaka paundi million 50 ikiwa na mshahara wake wa
kawaida poundi million 40 kwa mwaka zaidi anacho kipata pale Barcelona.
AS inaripoti kwa kusema kuwa Neymar ataondoka Catalona ili aweze kuwa
mchezaji bora dunia kwasababu akiendelea kukaa kwenye kivuli cha Lionel
Messi ataweza kuwa mchezaji bora duniani.
PSG wanafanya hivyo ili kupata mbadala wa Ibrahimovic aneondoka mwezi wa saba baada ya mkataba wake kuisha.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni