.

.

14 Mei 2015

MARAIS AFRIKA MASHARIKI WALAANI JARIBIO LA KUPINDULIWA NKURUNZINZA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe akizungumza na waandishi wa habari mapema leo asubuhi kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu J.K. Nyerere, jijini Dar es salaam.
Na Chalila Kibuda

MARAIS wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wamelaani kitendo cha baadhi ya askari kufanya jaribio la kutaka kuipindua serikali ya Burundi.
Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es salaam leo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe amesema kuwa hali ya Burundi ni tete na kwamba japo linaonekana ni jambo dogo lakini linaweza kugharimu maisha ya watu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni