.

.

20 Mei 2015

TAIFA STARS NJE YAPIGWA 2-0 NA MADAGASCAR



TANZANIA imeaga mashindano ya Kombe la COSAFA baada ya kufungwa manao 2-0 na Madagascar katika mchezo wa Kundi B jioni ya leo Uwanja wa Royal Bafokeng Sports Palace.
Huo unakuwa mchezo wa pili mfululizo timu hiyo kufungwa, baada ya awali kulala 1-0 mbele ya Swaziland Jumatatu na sasa itakamilisha ratiba Ijumaa kwa kumenyana na Lesotho kabla ya kurejea nyumbani.
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Duncan Lengani wa Malawi aliyesaidiwa na Arsenio Chadreque Marengula wa Msumbiji na Isaskar Boois wa Namibia, Madagascar walikwenda kupumzika wakiwa wanaongoza mabao 2-0.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni