.

.

28 Juni 2015

KAMANDA WA POLISI MORO AKANUSHA WATU WATATU KUUAWA

Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, SACP Leonard Paul.
Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, SACP Leonard Paul amekanusha kuwa habari zilizozagaa katika mitandao ya kijamii kuwa watu watatu wamefariki dunia wawili kati yao wanasadikiwa kuwa ni wafuasi wa Kundi la Kigaidi la Al Shabaab katika mapigano baina yao na jeshi la Polisi si kweli na kwamba hakuna mtu aliyefariki mkoani humo. Kamanda huyo, amelaani vikali tabia ya watu kuvumisha habari ambazo siyo za kweli kupitia mitandao ya kijamii.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni