.

.

10 Mei 2016

HAYA NDIYO ALIYOYASEMA STRAIKA WA TANZANIA PRISONS.



STRAIKA wa Prisons, Jeremiah Juma ameweka wazi kuwa hana papara ya kuondoka ndani ya kikosi hicho kwani hakuna timu inayoweza kununua ajira yake kwa sasa ingawa kuna timu zinamnyemelea.
Jeremiah ambaye pia aliitwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ kwa mara ya kwanza kilichokuwa kinajiandaa na mechi dhidi ya Chad ya kuwania kufuzu fainali za Afcon aliliambia Mwanaspoti kuwa anaamini umri wake bado unamruhusu kusubiri na kuendelea kuwemo kwenye kikosi cha Maafande hao hivyo kwa msimu huu hajafikiria kuondoka.
Alisema kuwa endapo ataondoka kwenda timu nyingine ambayo si ya kijeshi basi wawe wamemuandalia kitita cha maana ambacho kitamshawishi kuacha ajira hiyo ambayo ameitumikia kwa mwaka mmoja kati ya mkataba wa miaka mitatu.
“Si kwamba hakuna timu ambazo zimeonyesha nia, zipo nyingi tu ila siwezi kuzikubalia kutokana na dau ambalo huwa wananiambia, ni dau dogo sana ambalo haliendani na thamani ya ajira yangu, hivyo siwezi kuacha ajira na kukimbilia fedha ya msimu ambayo ni ndogo mno, muda ukifika na kwa fedha ya maana nitaweza kuondoka.
“Mkataba wangu ni kwamba siku nikiamua kuacha ajira basi na mkataba wa timu utakuwa umemalizika hapo yanakuwa ni makubaliano yangu na wanaonihitaji, ila kwasasa acha niendelee kuwepo hapa nikijijenga zaidi, ila nawashauri tu wachezaji kuwa kipindi hiki cha usajili wawe watulivu na wasikurupuke kutoa uamuzi,” alisema Jeremiah ambaye amefunga mabao 12 mpaka sasa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni