Dkt John Pombe Joseph Magufuli aliingia ofisini Novemba 5,2015 akiwa Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Dkt Magufuli
ndani ya siku hizi takribani 100 amejizolea umaarufu mkubwa mitandaoni
na duniani Kwa wananchi waliowengi Kwa namna anavyochapa Kazi
unaonogeshwa na kauli mbiu yake ya HAPA KAZI TU!
Dkt Magufuli
ameonekana kujikita zaidi katika kushughulikia matatizo ya msingi ya
nchi hasa vitendo vya ufisadi wa rasilimali za Taifa, Ubanaji wa
matumizi serikalini, upatikanaji wa huduma za jamii, uimarishaji wa
miundombinu, kuzuia ukwepaji kodi TRA na TPA n.k
MAAJABU YA SIKU 100 ZA DKT MAGUFULI
1. Alifuta
vitengo vya mapokezi na lishe Ikulu punde baada ya kuingia ofisini na
kuwarejesha watendaji husika katika wizara mama walizotoka.
2. Aliweka mkazo
katika kuzuia na kupambana na ukwepaji kodi TRA na TPA ili kuongeza
ukusanyaji mapato. Hapa vigogo kadhaa walionekana hawatamudu kasi ya
HAPA KAZI TU walisimamishwa Kwa uchunguzi na wengine kufukuzwa huku
hatua za kisheria zikichukuliwa dhidi yao.
3. Kubana
matumizi ili kuhakikisha serikali inapata fedha za kuendesha miradi ya
maendeleo, kuimarisha na kuboresha upatikanaji wa huduma Kwa wananchi
waliowengi. Mifano ya Ubanaji matumizi ni:-
(a) Aliagiza
zaidi ya shilingi million 200 zilizokuwa zitumike katika hafla ya
uzinduzi wa bunge zikatumike kununulia vitanda vya wagonjwa hospitali
kuu ya Taifa ya Muhimbili ambapo vitanda 300 vilinunuliwa.
(b) Alifuta
shamrashamra za maadhimisho ya sherehe za uhuru wa (Tanganyika) Tanzania
Bara Disemba 9, 2015 ambapo aliokoa shilingi billion 4.2 fedha
zilizoelekezwa kufanya upanuzi wa barabara ya Morocco - Mwenge ambao
unaendelea.
(c) Amepiga
marufuku safari za nje Kwa mawaziri, viongozi waandamizi wa serikali na
hata katika mashirika ya umma pasipo kibali cha Ikulu huku akiagiza
mabalozi wa Tanzania katika nchi husika kuiwakilisha serikali yake huko.
Katika eneo hili ameokoa zaidi ya shilingi billion 3.5 Kwa kuacha
kusafiri safari tano ambazo ni:-
(i) Novemba
27,2015 mkutano wa wakuu wa nchi wa jumuiya ya madola (CHOGM)
uliofanyika visiwa vya Malta. Badala yake Tanzania iliwakilishwa na
balozi wa Tanzania Uingereza na maafisa watatu.
(ii) Novemba 29,
2015 mkutano wa kimataifa wa 21 wa kujadili mabadiliko ya tabianchi
Duniani (COP21) uliofanyika Paris, ufaransa. Ulihudhuriwa na Marais 150
kati ya 195 wakiwamo Barack Obama na Xi Jinping. Tanzania iliwakilishwa
na balozi.
(iii) Disemba 5,
2015 mkutano wa tano wa wakuu wa nchi wa Afrika na Rais wa China Xi
Jinping kupitia jukwaa la nchi za Afrika na China (FOCAC). Tanzania
ilihali na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan.
(iv) Mkutano wa
wakuu wa nchi za Maziwa makuu (SADC) uliofanyika Gaborone, Botswana.
Tanzania iliwakilishwa na Waziri Mkuu Ndg Majaliwa Kassim Majaliwa.
(v) Mkutano wa
Umoja Wa Afrika (AU) uliowakutanisha wakuu wa nchi za Afrika ulifanyika
Addis Ababa, Ethiopia. Tanzania iliwakilishwa na Makamu wa Rais Mama
Samia Suluhu Hassan na Balozi Agustine Mahiga.
Katika kuonesha
hana masihara na agizo hili serikali iliwasimamisha Kazi watumishi wanne
wa TAKUKURU Kwa kwenda nje ya nchi pasipo kibali maalum cha Ikulu.
Fahamu msafara wa Rais wa JMT kwenda nje ya nchi huwa na Watu kuanzia 50 ambapo huitajika zaidi ya million 700 kuwahudumia
Dkt Magufuli amesafiri nje ya Dar es Salaam mara 5 huku akiwa amepanda ndege mara mbili tu!
4. Aliapisha
baraza la mawaziri na wateule wake wakiwamo makatibu wakuu wa wizara na
manaibu wao bila shamrashamra wala mbwembwe kama ilivyozoeleka huku
wahusika wakifika Ikulu kuapa bila kuambatana na utitiri wa ndugu na
jamaa ambao wangewalaki Kwa maua na mashada baada ya kuapishwa.
5. Amefuta umiliki wa mashamba 17 makubwa ambayo hayaendelezwa na kuyarejesha serikalini.
6. Wananchi wa
mataifa mengi Duniani wanapaza sauti kila kukicha wakizitaka serikali
zao kumuiga Dkt Magufuli mfano Australia walimtaka waziri mkuu wao
kumuiga katika kubana matumizi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni