.

.

02 Agosti 2016

DC ILALA,SOPHIA MJEMA AZINDUA UWANJA WA NETIBOLI NA KIKAPU SHULE YA JANGWANI JIJINI DAR LEO

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema akifunga goli wakati wa uzinduzi wa uwanja wa Netiboli na Mpira wa Kikapu wa Shule ya Sekondari ya Jangwani uliojengwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Kidoti, Jokate Mwegelo kupitia kampeni yake ya "Be Kidotified".  Mjema alizindua uwanja huo leo katika hafla fupi iliyofanyika katika shule hiy.Kushoto ni Jokate akishuhudia tukio hilo.PICHA NA MICHUZI JR
  Mkuu wa  Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema (kushoto) akitoa hotuba yake katika hafla fupi ya uzinduzi wa uwanja wa mpira wa kikapu na netiboli uliojengwa na mrembo, Jokate Mwegelo (kushoto). Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Mo Dewji Foundation, Barbara Gonzalez akifuatiwa na Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL, Fatema Dewji na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema na wa Mwisho ni Mkuu wa Shule Msaidizi wa shule ya Jangwani, Amos Mgongolwa.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Kidoti, Jokate Mwegelo (Kushoto) akizungumza katika halfa ya uzinduzi wa uwanja alioujenga kupitia kampeni yake ya "Be Kidotified" uliomgharimu kiasi cha Sh Milioni 50. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Mo Dewji Foundation, Barbara Gonzalez akifuatiwa na Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL, Fatema Dewji na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema na wa Mwisho ni Mkuu wa Shule Msaidizi wa shule ya Jangwani, Amos Mgongolwa. 
Mrembo wa zamani wa Tanzania, Faraja Kota akizungumza mbele ya Wanafunzi katika hafla fupi ya uzinduzi wa uwanja wa mpira wa kikapu na netiboli uliojengwa na mrembo, Jokate Mwegelo. 
 Mandhari ya uwanja wa Mpira wa Kikapu na Netiboli wa shule ya Sekondari ya Jangwani uliojengwa na Mrembo, Jokate Mwegelo kupitia kampeni yake ya "Be Kidotified".
Mkuu wa Wilaya ya Ilala pichani kati Mh.Sophia Mjema akiwasili kwenye hafla fupi ya uzinduzi wa uwanja wa mpira wa Netiboli na Kikapu wa shule ya Jangwani leo jijini Dar,Pichani kulia ni Katibu Tawala wilaya ya Ilala.Ndugu Edward Mpogolo na kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Kidoti, Jokate Mwegelo.

 Akizungumza katika uzinduzi huo, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema alisema kuwa amefurahishwa na mpango huo wa Jokate kwa kusaidiana na Mo Dewji Foundation na kuwaomba kuuendeleza kwa shule nyingineza jijini.

Mjema alisema kuwa Dar es Salaam kuna shule nyingi na angependa kuona hata shule za Chanika zinafaidika na kampeni ya "Be Kidotified". Alisema kuwa amefarijika sana kuona shule aliyosoma yeye kufaidika kwa mradi huo na kuwaomba wanafunzi na walimu kuutumia uwanja huo kama fursa ya kuendeleza michezo na taaluma.

Wakati huo huo Mrembo mwenye vipaji lukuki, Jokate Mwegelo kupitia kampeni yake ya kuchangia jamii ijulikanayo kwa jina la “Be Kidotified” amejenga uwanja utakaotumika kwa ajili ya michezo ya mpira wa kikapu na Pete (netiboli) kwa Shule ya Sekondari ya Wasichana wa Jangwani. 

Uwanja huo ulizinduliwa jijini leo katika hafla fupi iliyofanyika kwenye shule hiyo na kuhudhuriwa na wanafunzi, walimu na viongozi mbalimbali wa serikali. Ujenzi wa uwanja huo umemgharimu Jokate kiasi cha Shilingi milioni 50.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Jokate alisema kuwa ameamua kuonyesha mfano kupitia ‘Kidoti Brand’ kuchangia maendeleo ya michezo nchini hasa kwa katika shule ambazo ni kiini cha maendeleo ya sekta hiyo hapa nchini. Mbali ya michezo, pia Kidoti Brand inajihusisha zaidi na maendeleo ya elimu hapa nchini. 

Alisema kuwa serikali ya awamu ya tano ya Tanzania imeadhimia kuondoa changamoto nyingi katika elimu na yeye kuamua kuanzia katika masuala ya michezo ambayo uchangia ufaulu darasani na kuibua vipaji ambavyo vitamwezesha mshiriki kupata ajira. 

Alisema kuwa moja ya changamoto kubwa zinazorudisha nyuma maendeleo ya michezo nchini ni ukosefu wa viwanja bora ambavyo ukwamisha wachezaji chipukizi kuonyesha vipaji vyao ipasavyo. 

Kwa mujibu waJokate, alipokuwa anasoma, alikutana na changamoto hizo, lakini alipiga moyo konde na kujihusisha na shughuli mbalimbali za nje ya darasa ikiwa pamoja na michezo na kujifunza mengi. 

“Mimi ni mjasiriamali mchanga sana hapa nchini, nimehamasisha kwa kile kidogo nilichonacho na kwa msaada wa wadhamini niliyotafuta kuhitimisha ujenzi wa uwanja huu ambao utatumika si kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Jangwani pekee, bali hata kwa mechi za shule nyingine, ” 

“Nawapongeza wadhamini walioniunga mkono katika mpango huu kama Mo Dewji Foundation, na wadau ambao walikuwa nyuma yangu katika kuhakikisha kampeni ya ‘Be Kidotified’ inaanza kwa mafanikio makubwa na kuendelea kwa shule nyingine za hapa jijini,” alisema Jokate. 

Alisema kuwa chapa ya Kidoti ni miongoni mwa chama zinazoongoza hapa nchini katika mitindo, urembo na burudani kabla ya kuamua kupanua wigo kwa upande wa michezo tofauti na mpira wa miguu. 

Alifafanua kuwa alianza kwa kuanzisha kampuni ya Kidoti (Kidoti Company) na kuchangia katika soko la ajira nchini na baadaye kuanzisha “kidoti brand’ akiwa na lengo la kuhamasisha vijana kujihusisha katika shughuli mbalimbali za ujasiriamali ili kuweza kukabiliana na maisha ya ki
la siku.

KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, leo asubuhi imeanza tena mazoezi yake baada ya mapumziko ya jana huku ikitarajia kucheza mechi mbili za kirafiki kwa mujibu wa programu ya wiki hii.

Azam FC ilipumzika jana Jumatatu ili kuondoa uchovu wa kambi ya Zanzibar, ambayo ilikuwa ni sehemu ya muendelezo wa maandalizi ya msimu ujao unaotarajia kuanza Agosti 17, mwaka huu kwa kucheza mchezo wa Ngao ya Hisani dhidi ya Yanga.

Mabingwa hao katika programu ya wiki hii wataendelea kucheza mechi za kirafiki, ambapo kesho Jumatano saa 10.00 jioni itacheza na JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Azam Complex.

Mbali na mchezo huo, Jumamosi ijayo itakipiga na Ruvu Shooting nyumbani kwao kwenye Uwanja wa Mabatini, Pwani, mechi ambayo itafunga maandalizi ya Azam FC wiki hii kabla ya kupumzika Jumapili ijayo.

Mpaka sasa Azam FC imeshacheza mechi tano za kirafiki zote ikishinda kwa kuzilaza, Friends Rangers (2-1), Ashanti United (1-0), Mshikamano (1-0), Wilaya ya Mjini (1-0) na Taifa ya Jang’ombe (1-0).  

Kikosi hicho kinakaribia kufikisha mwezi sasa tokea kilipoanza kufundishwa na makocha wapya kutoka Hispania, Kocha Mkuu Zeben Hernandez, Msaidizi wake, Yeray Romero, Kocha Mkuu wa Viungo, Jonas Garcia, Msaidizi wake, Pablo Borges, Kocha wa Makipa, Jose Garcia na Mtaalamu wa Viungo, Sergio Perez Soto.
- See more at: http://www.barakampenja.com/2016/08/mechi-nyingine-za-kujipima-nguvu-za.html#sthash.BwJTH2z7.Iq19UWOQ.dpuf

KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, leo asubuhi imeanza tena mazoezi yake baada ya mapumziko ya jana huku ikitarajia kucheza mechi mbili za kirafiki kwa mujibu wa programu ya wiki hii.

Azam FC ilipumzika jana Jumatatu ili kuondoa uchovu wa kambi ya Zanzibar, ambayo ilikuwa ni sehemu ya muendelezo wa maandalizi ya msimu ujao unaotarajia kuanza Agosti 17, mwaka huu kwa kucheza mchezo wa Ngao ya Hisani dhidi ya Yanga.

Mabingwa hao katika programu ya wiki hii wataendelea kucheza mechi za kirafiki, ambapo kesho Jumatano saa 10.00 jioni itacheza na JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Azam Complex.

Mbali na mchezo huo, Jumamosi ijayo itakipiga na Ruvu Shooting nyumbani kwao kwenye Uwanja wa Mabatini, Pwani, mechi ambayo itafunga maandalizi ya Azam FC wiki hii kabla ya kupumzika Jumapili ijayo.

Mpaka sasa Azam FC imeshacheza mechi tano za kirafiki zote ikishinda kwa kuzilaza, Friends Rangers (2-1), Ashanti United (1-0), Mshikamano (1-0), Wilaya ya Mjini (1-0) na Taifa ya Jang’ombe (1-0).  

Kikosi hicho kinakaribia kufikisha mwezi sasa tokea kilipoanza kufundishwa na makocha wapya kutoka Hispania, Kocha Mkuu Zeben Hernandez, Msaidizi wake, Yeray Romero, Kocha Mkuu wa Viungo, Jonas Garcia, Msaidizi wake, Pablo Borges, Kocha wa Makipa, Jose Garcia na Mtaalamu wa Viungo, Sergio Perez Soto.
- See more at: http://www.barakampenja.com/2016/08/mechi-nyingine-za-kujipima-nguvu-za.html#sthash.BwJTH2z7.Iq19UWOQ.dpuf

KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, leo asubuhi imeanza tena mazoezi yake baada ya mapumziko ya jana huku ikitarajia kucheza mechi mbili za kirafiki kwa mujibu wa programu ya wiki hii.

Azam FC ilipumzika jana Jumatatu ili kuondoa uchovu wa kambi ya Zanzibar, ambayo ilikuwa ni sehemu ya muendelezo wa maandalizi ya msimu ujao unaotarajia kuanza Agosti 17, mwaka huu kwa kucheza mchezo wa Ngao ya Hisani dhidi ya Yanga.

Mabingwa hao katika programu ya wiki hii wataendelea kucheza mechi za kirafiki, ambapo kesho Jumatano saa 10.00 jioni itacheza na JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Azam Complex.

Mbali na mchezo huo, Jumamosi ijayo itakipiga na Ruvu Shooting nyumbani kwao kwenye Uwanja wa Mabatini, Pwani, mechi ambayo itafunga maandalizi ya Azam FC wiki hii kabla ya kupumzika Jumapili ijayo.

Mpaka sasa Azam FC imeshacheza mechi tano za kirafiki zote ikishinda kwa kuzilaza, Friends Rangers (2-1), Ashanti United (1-0), Mshikamano (1-0), Wilaya ya Mjini (1-0) na Taifa ya Jang’ombe (1-0).  

Kikosi hicho kinakaribia kufikisha mwezi sasa tokea kilipoanza kufundishwa na makocha wapya kutoka Hispania, Kocha Mkuu Zeben Hernandez, Msaidizi wake, Yeray Romero, Kocha Mkuu wa Viungo, Jonas Garcia, Msaidizi wake, Pablo Borges, Kocha wa Makipa, Jose Garcia na Mtaalamu wa Viungo, Sergio Perez Soto.
- See more at: http://www.barakampenja.com/2016/08/mechi-nyingine-za-kujipima-nguvu-za.html#sthash.BwJTH2z7.Iq19UWOQ.dpuf

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni